Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 8 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 86 | 2026-04-14 |
Name
Emmanuel Peter Cherehani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Primary Question
MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: -
Je, upi mpango wa kupunguza tozo kwa wakulima wa tumbaku, kwani kwa kila mfuko wa mbolea, benki hukata USD 0.5 na Benki Kuu USD 5.80?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani, Mbunge wa Jimbo la Ushetu, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha kilimo cha zao la tumbaku ili kuongeza uzalishaji na tija kwa mkulima kwa kuimarisha mapato ya mkulima na kupunguza gharama za uzalishaji wa zao hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa, Serikali ipo kwenye hatua ya kupitia gharama za uzalishaji za mkulima ili kuainisha maeneo ambayo yanahitaji kufanyiwa maboresho ikiwemo riba za kibenki ambayo ni dola za Kimarekani 0.5 kwa mfuko wa mbolea ikiwa ni ada ya hati ya dhamana ya benki iliyotoa mkopo pamoja na dola za Kimarekani 5.8 inayojumuisha riba ya mkopo, dhamana ya Benki Kuu, bima ya mkopo na kodi ya ongezeko la thamani. Aidha, jitihada hizo zitaenda sambamba na kushirikisha Benki zinazotoa mikopo hiyo kwa wakulima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Bodi ya Tumbaku na Tume ya Maendeleo ya Ushirika, zitaendelea na jitihada za kuboresha mazingira ya uzalishaji kwa wakulima wa zao la tumbaku ikiwemo kuboresha tija na kuainisha tozo ambazo zinahitaji kufanyiwa maboresho ili kuweza kupunguza gharama za uzalishaji kwa wakulima wa zao hilo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved