Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 8 | Works, Transport and Communication | Wizara ya Uchukuzi | 85 | 2026-04-14 |
Name
Janeth Elias Mahawanga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -
Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha wanawake wanashiriki katika miradi mikubwa ya uchukuzi, ikiwemo Mradi wa SGR?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeweka sera, sheria na miongozo mbalimbali inayolenga kuhimiza na kuhakikisha usawa wa kijinsia katika ajira. Katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati, ikiwemo ujenzi wa SGR, wakandarasi na washauri wanawajibika kuzingatia masharti ya mikataba, pamoja na sera za Kitaifa ambazo zinataka utoaji wa fursa sawa za ajira kwa wanawake na wanaume katika kada mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa masharti ya mikataba ya ujenzi inayotumika katika Ujenzi wa SGR, mkandarasi na mshauri, wanatakiwa kufuata sheria zote za nchi, zikiwemo zile zinazohusu ajira, kazi na usawa wa kijinsia. Hivyo, Serikali imeendelea kusisitiza utekelezaji wa matakwa haya ili kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika miradi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia, inaendelea kufanya ufuatiliaji na tathmini ya mara kwa mara ya utekelezaji wa sera na miongozo hiyo kwa lengo la kuhakikisha kuwa, malengo ya usawa wa kijinsia yanafikiwa na wanawake wanapata fursa stahiki za kushiriki katika miradi mikubwa ya kimaendeleo nchini.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved