Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 73 2026-04-13

Name

Amina Ali Mzee

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza gati katika Bandari ya Dar es Salaam ili kuhudumia meli nyingi zaidi?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Ali Mzee, Mbunge wa Vitu Maalum Vijana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia utekelezaji wa Mradi wa DMGP (Dar es Salaam Maritime Gate Project) katika Bandari ya Dar es Salaam unaoendelea ambao umehusisha uboreshaji wa gati nane kuanzia gati namba sifuri hadi gati namba saba, ikiwa ni pamoja na uongezaji wa kina cha lango la kuingilia meli (Entrance Channel) hadi kufikia meta 14.5 na lango la kugeuzia meli (Turning Basin), mradi huu umechangia kuongeza ufanisi na uwezo wa kuhudumia meli kubwa zaidi kuliko hapo awali na hivyo kuongeza idadi ya meli na kiasi cha shehena inayohudumiwa na Bandari hiyo kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inaratibu mpango wa ujenzi wa gati mpya zipatazo 10 ili kuhudumia meli nyingi zaidi kwa wakati mmoja.