Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 7 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 73 | 2026-04-13 |
Name
Amina Ali Mzee
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza gati katika Bandari ya Dar es Salaam ili kuhudumia meli nyingi zaidi?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Ali Mzee, Mbunge wa Vitu Maalum Vijana, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia utekelezaji wa Mradi wa DMGP (Dar es Salaam Maritime Gate Project) katika Bandari ya Dar es Salaam unaoendelea ambao umehusisha uboreshaji wa gati nane kuanzia gati namba sifuri hadi gati namba saba, ikiwa ni pamoja na uongezaji wa kina cha lango la kuingilia meli (Entrance Channel) hadi kufikia meta 14.5 na lango la kugeuzia meli (Turning Basin), mradi huu umechangia kuongeza ufanisi na uwezo wa kuhudumia meli kubwa zaidi kuliko hapo awali na hivyo kuongeza idadi ya meli na kiasi cha shehena inayohudumiwa na Bandari hiyo kwa mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inaratibu mpango wa ujenzi wa gati mpya zipatazo 10 ili kuhudumia meli nyingi zaidi kwa wakati mmoja.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved