Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 71 2026-04-13

Name

Faraji Buriani Nandala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. FARAJI B. NANDALA aliuliza: -

Je, lini Wananchi wa Kata za Chikukwe, Chigugu, Chikundi, Mwena, Ndanda na Nanganga ambao wamepitiwa na Mradi wa Grid ya Taifa watalipwa fidia?

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Faraji Buriani Nandala Mbunge wa Ndanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka huu wa fedha wa 2025/2026 Serikali imetenga bajeti kwa ajili ya malipo ya fidia yenye thamani ya shilingi bilioni 5.1 kwa wananchi 1,730 wanaopisha njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 220 kutoka Masasi hadi Mahumbika. Hivyo, naomba kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kuwa fidia hii italipwa mwaka huu wa fedha kadri itakavyopatikana.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Faraji Buriani Nandala.