Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 7 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 68 2026-04-13

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI K.n.y. MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha vikundi vya wanawake kiuchumi katika Mkoa wa Ruvuma ili wapate fursa za masoko, mafunzo na mitaji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nyoka, Mbunge wa Viti Maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inashirikiana na wadau kutekeleza mikakati ya kuendeleza vikundi vya wanawake kiuchumi kwenye mikoa yote, ambapo kwa Mkoa wa Ruvuma jumla ya vikundi vya kiuchumi 9,430 vya wanawake vimeshasajiliwa na usajili unaendelea. Baada ya usajili wa vikundi hivyo, mikakati ifuatayo inaendelea ili kuiimarisha viweze kukidhi kupata mitaji:-

(i) Kutoa elimu na mafunzo ya ujasiriamali ili vikundi viwe na uwezo wa kujiendesha na kutekeleza miradi yenye uendelevu inayokuza ajira na kuongeza kipato;

(ii) Kutoa elimu ya mikopo ikiwemo ile isiyo na riba kuanzia iliyopo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa na kwenye Taasisi za umma na binafsi;

(iii) Kuendelea kurasimisha biashara za wanawake ambapo kupitia mkakati huu, vikundi vinaendelea kuelimishwa na kusajili biashara zao ili zitambulike kisheria, kupata sifa ya kukopesheka na ukubalifu katika masoko ya ndani na nje;

(iv) Ushirikishwaji wa vikundi kwenye fursa ya kujitangaza, kuongeza wigo wa wateja, kubadilishana uzoefu na kupata masoko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya ukuaji wa vikundi vya wanawake kiuchumi.