Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 7 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 66 | 2026-04-13 |
Name
John Stephano Luhende
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. JOHN S. LUHENDE aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji kwa ajili ya kilimo cha kisasa katika eneo la Kisasiga Jimbo la Bukene?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na utekelezaji wa miradi ya umwagiliaji katika maeneo mbalimbali katika Mkoa wa Tabora ikiwemo Jimbo la Bukene. Kwa mwaka 2025/2026, jumla ya miradi nane ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika Jimbo la Bukene inaendelea, ambapo utekelezaji wa miradi hiyo umefikia wastani wa asilimia 39.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi hiyo ni Kahamanhalanga, Mambali, Ikindwa, Malolo, Igombe, Lakuyi, Nindo na Sigili. Kukamilika kwa upembuzi yakinifu na usanifu, kutaiwezesha Serikali kujua gharama halisi kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa ya umwagiliaji pamoja na kuimarisha miundombinu ya mashambani ili kuwezesha kufanyika kwa kilimo chenye tija.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika mwaka 2026/2027 imepanga kufanya tathmini katika eneo la Kisasiga kwa lengo la kubaini mahitaji halisi ya miundombinu ya umwagiliaji. Baada ya kukamilika kwa tathmini hiyo, mradi huu utaingizwa katika mipango ya Serikali kwa ajili ya utekelezaji.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved