Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 66 2026-04-13

Name

John Stephano Luhende

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. JOHN S. LUHENDE aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji kwa ajili ya kilimo cha kisasa katika eneo la Kisasiga Jimbo la Bukene?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na utekelezaji wa miradi ya umwagiliaji katika maeneo mbalimbali katika Mkoa wa Tabora ikiwemo Jimbo la Bukene. Kwa mwaka 2025/2026, jumla ya miradi nane ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika Jimbo la Bukene inaendelea, ambapo utekelezaji wa miradi hiyo umefikia wastani wa asilimia 39.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi hiyo ni Kahamanhalanga, Mambali, Ikindwa, Malolo, Igombe, Lakuyi, Nindo na Sigili. Kukamilika kwa upembuzi yakinifu na usanifu, kutaiwezesha Serikali kujua gharama halisi kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa ya umwagiliaji pamoja na kuimarisha miundombinu ya mashambani ili kuwezesha kufanyika kwa kilimo chenye tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika mwaka 2026/2027 imepanga kufanya tathmini katika eneo la Kisasiga kwa lengo la kubaini mahitaji halisi ya miundombinu ya umwagiliaji. Baada ya kukamilika kwa tathmini hiyo, mradi huu utaingizwa katika mipango ya Serikali kwa ajili ya utekelezaji.