Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 65 2026-04-13

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: -

Je, lini Barabara ya Kilolo – Udekwa – Ilula itakamilika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kilolo – Udekwa – Ilula ni barabara ya mkoa inayojulikana kwa jina la Kilolo – Ipalamwa – Watalisoli – Ilula yenye urefu wa kilometa 91. Kwa sasa, Serikali ipo katika hatua za mwisho za manunuzi ya kumpata mhandisi mshauri wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi.