Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 7 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 64 | 2026-04-13 |
Name
Sara Msafiri Ally
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Mvomero
Primary Question
MHE. SARA M. ALLY aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Kipera – Mlali – Nyandila – Luale – Kikeo hadi Kisaki kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Sara Msafiri Ally, Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kipera – Mlali – Nyandila – Luale – Kikeo – Kisaki inajumuisha barabara ya Mkoa ambayo inaanzia Sangasanga – Langali – Luale – Kikeo yenye urefu wa kilometa 59.16 inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha barabara hiyo inapitika majira yote ya mwaka na kutoa huduma ya usafiri na usafirishaji kwa wananchi, Serikali imeendelea kufanya matengenezo mbalimbali hususan sehemu korofi kwa kuijenga kwa kiwango cha lami na zege ambapo jumla ya kilometa 13.19 zimejengwa na kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali pamoja na hatua hizo, inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hiyo ili kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved