Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 2 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 10 2026-04-01

Name

Esther Nicholas Matiko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kiwanda cha kimkakati ndani ya Mji wa Tarime?

Name

Denis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Viwanda na Biashara naomba nijibu swali namba 10 la Mheshimiwa Esther Matiko.

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wake Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, tunafanya kazi, na tumeandaa mpango wa ujenzi wa Viwanda nchini katika kuongeza thamani ya bidhaa zetu ikiwemo Mji wa Tarime ambapo itazingatia uongezaji wa thamani katika mazao ya kilimo, mifugo na madini ambayo yanapatikana huko.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali inaendelea kuhamasisha uwekezaji wa ndani na nje katika ujenzi wa viwanda vidogo, vya kati na vikubwa vyenye mkakati kupitia Taasisi za TISEZA na SIDO. Wakati huo huo tunahamasisha balozi zetu, wadau mbalimbali na wananchi wote wa Tanzania kwa pamoja kutangaza rasilimali na vivutio ambavyo vipo katika Mji wa Tarime na Mkoa wa Mara kwa ujumla ili hamasa hiyo iende sambamba na kutoa vivutio vya kikodi na visivyo kikodi ambavyo vinaendelea kutolewa chini ya Taasisi ya TISEZA.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.