Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 9 2026-04-01

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kupeleka Mradi wa Majisafi Kata ya Mpinji kwa Vijiji vyote vinne?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Same Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kwamba vijiji vyote 12,333 vilivyopo nchini vinafikiwa na huduma ya majisafi na salama kufikia mwaka 2030. Aidha, hadi sasa jumla ya vijiji 10,758 vimeshafikishiwa huduma ya majisafi na salama kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA).

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kufikisha huduma ya maji katika vijiji 1,575 vilivyobaki, ikiwemo vijiji vinne vya Mpinji, Sambweni, Kirongwe na Ivuga vilivyopo Kata ya Mpinji Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro.