Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 5 2026-04-01

Name

Enock Zadock Koola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ENOCK Z. KOOLA aliuliza :-

Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji kwa ajili ya kilimo cha chakula katika Jimbo ya Vunjo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umwagiliaji katika Mkoa wa Kilimanjaro ikiwemo Jimbo la Vunjo. Kwa mwaka 2025/2026, miradi mitano inaendelea kutekelezwa katika Jimbo la Vunjo ikihusisha mradi wa ujenzi wa Skimu ya Mawala wenye ukubwa wa hekta 2,500 unaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 4.1.

Mheshimiwa Spika, vilevile, miradi minne imepangwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha ujao wa 2026/2027 inayojumuisha skimu nne za Mananga, Ndekambeko, Masaera na Masaga ambapo mkandarasi ameshapatikana.