Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 3 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 19 2026-04-02

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga daraja litakalounganisha Tarafa ya Mkongo kati ya Kata ya Mkongo na Utete ambayo ni Makao Makuu ya Wilaya ya Rufiji?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa daraja unahusisha hatua mbalimbali ikiwemo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya usanifu wa daraja linalounganisha Kata ya Mkongo na Utete. Kazi hiyo itakapokuwa imekamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa daraja hilo, ahsante.