Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 3 | Information, Culture, Arts and Sports | Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo | 17 | 2026-04-02 |
Name
Kassimu Amari Mbaraka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tanga Mjini
Primary Question
MHE. KASSIMU A. MBARAKA aliuliza: -
Je, lini Serikali itafunga viti katika Uwanja wa Mpira wa Mkwakwani – Tanga kwa kuwa viti vimepelekwa na vipo uwanjani?
Name
Hamis Mohamed Mwinjuma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muheza
Answer
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo inakipongeza Chama cha Mapinduzi pamoja na wadau wengine zikiwemo halmashauri mbalimbali na taasisi binafsi nchini kwa kuwa wadau muhimu katika kukuza na kuendeleza michezo, na hasa kwa kujenga na kutunza miundombinu mbalimbali ya michezo, hususan viwanja vya michezo ya kipaumbele; mathalan mpira wa miguu, mpira wa netiboli, mpira wa kikapu, na mpira wa wavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, viwanja hivi kikiwemo kiwanja cha Mkwakwani vimekuwa vikitumika katika kuendesha ligi kuu na mashindano mengine mbalimbali nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iliwezesha upatikanaji wa viti 6,500 vilivyotolewa uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam wakati ukifanyiwa ukarabati, ambapo vilikabidhiwa kwa uongozi wa CCM Mkoa wa Tanga kwa ajili ya kufungwa katika uwanja wa Mkwakwani. Kwa sasa uongozi wa CCM Mkoa wa Tanga umeshapata mtaalamu wa kufunga viti hivyo, na kazi inaendelea.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved