Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 16 2026-04-02

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka fedha za kukamilisha ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kayanga?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Lugha Bashungwa, Mbunge wa Karagwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi miwili ya maji katika Mji wa Kayanga Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera. Miradi hiyo ni pamoja na Mradi wa Miji 28 wa Rwakajunju unaotekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 64.3 sambamba na mradi wa usambazaji maji katika Mji wa Kayanga unaogharimu jumla ya shilingi bilioni 1.31.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hiyo kwa pamoja utekelezaji wake umefikia wastani wa 70%, ambapo inalenga kunufaisha zaidi ya wananchi 356,790 waishio kwenye Mji wa Kayanga wilayani Karagwe. Hadi kufikia mwezi Machi, 2026, Serikali imelipa jumla ya shilingi bilioni 42.98 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kupeleka fedha za utekelezaji wa mradi huo kulingana na hati za madai zinazowasilishwa na mkandarasi.