Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 3 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 13 | 2026-04-02 |
Name
Hawa Subira Mwaifunga
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya kutoka Kata ya Uyui - Kakola hadi Ikomwa?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Tabora Mjini, Mbunge wa Jimbo, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Tabora ina mtandao wa barabara wa jumla ya kilometa 775.64. Kati ya hizo, kilometa 61.9 ni tabaka la lami, kilometa 143.52 ni tabaka la changarawe. Barabara hii ya Uyui – Kakola – Ikomwa yenye Urefu wa kilometa 19 inaunganisha Kata tatu za Uyui - Kakola na Ikomwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye bajeti ya mwaka 2021/2022 barabara hii imetengewa fedha ya ukarabati. Mkandarasi wa kutekeleza kazi hii anaitwa AHAM Investment Company Limited ambapo kwa sasa yupo katika hatua za awali za kuanza kazi ambayo itadumu kwa mkataba wa miezi sita.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved