Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 12 2026-04-02

Name

Juma Ramadhani Mustafa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. JUMA R. MUSTAFA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa Daraja la Loya ili liweze kupitika muda wote na kuruhusu shughuli za kijamii?

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Ramadhani Mustafa, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilitoa shilingi milioni 318.9 kwa ajili ya kumlipa Mhandisi Mshauri aliyefanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Daraja hilo la Loya pamoja na madaraja mengine manne katika barabara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya usanifu imekamilika ambapo shilingi bilioni 26.68 zinahitajika kuweza kujenga daraja hilo lenye urefu wa meta 80 pamoja na madaraja mengine madogo manne. Taarifa zote za usanifu pamoja Kibali cha Mazingira kutoka NEMC tayari kimeshapatikana kwa ajili ya kuruhusu ujenzi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali imetenga shilingi bilioni 10 kupitia Mradi wa Urejeshaji wa Miundombinu katika maeneo yaliyoathirika na maafa ya mvua za mwaka 2024, chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, ujenzi wa madaraja mengine manne utafanyika kadiri fedha zitakapopatikana. Kwa sasa TARURA ipo katika hatua ya mwisho ya kumpata Mhandisi Msimamizi wa kazi hiyo na kazi ya ujenzi wa daraja hilo inatarajiwa kuanza kabla ya mwezi Mei, 2026.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.