Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 11 2026-04-02

Name

Chacha Mwita Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CHACHA M. WAMBURA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga na kukarabati mitaro katika Mitaa ya Mbugani na Kivukoni Geita ili kupunguza athari za mafuriko?

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Chacha Mwita Wambura, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya maeneo ya Mbugani na Kivukoni yana uelekeo wa maji mengi, hivyo hutokea mafuriko hasa nyakati za mvua nyingi. Ili kukabiliana na hali hiyo, tarehe 12 Disemba, 2025 ilifanyika tathmini ya awali kubaini chanzo cha mafuriko yanayotokea hasa nyakati za mvua za masika pamoja na kujiridhisha na hali ya miundombinu iliyopo hususan uwezo wa mitaro inayotiririsha maji katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tathmini hiyo ilibaini uhitaji wa upanuzi wa baadhi mitaro ili kuruhusu maji mengi yaweze kupita kwa urahisi kuanzia eneo la stendi kuu ya mabasi kuelekea katika maeneo ya Mbugani hadi Kivukoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, TANROADS kupitia kwa Mkandarasi Ms. Yamma Contractors Co. Ltd anaendelea na upanuzi wa mitaro hasa katika maingilio ya maji maeneo ya Shilabela pembezoni mwa barabara kuu ya Mwanza – Geita kwa gharama ya shilingi milioni 460.

Mheshimiwa Naibu Spika, shughuli hiyo kwa mujibu wa mkataba inatarajiwa kukamilika tarehe 15 Mei, 2026. Aidha, Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) inaendelea kufanya tathmini ya kina kubainisha gharama za upanuzi wa mitaro katika maeneo ya Mbugani na Kivukoni. Baada ya tathmini hiyo ambayo itakamilika mwezi Mei, 2026 Serikali itaanza upanuzi wa mitaro hiyo kulingana na upatikanaji wa fedha.