Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 53 | Water and Irrigation | Wizara ya Ujenzi | 687 | 2025-06-25 |
Name
Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Vwawa
Primary Question
MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza kusambaza maji katika Vijiji vya Hatete, Ihowa, Welu II, Ruanda na Myovizi – Vwawa?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji Hatete - Ruanda uliopo Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe. Kazi zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa tanki la maji lenye ujazo wa lita 200,000, ujenzi wa dakio (intake), ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 25 sanjari na ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 55% na unatarajiwa kukamilika mwezi Disemba, 2025 na kunufaisha wananchi 6,628 waishio kwenye vijiji vitano vya Hatete, Ruanda, Ihowa, Myovizi na Welu II.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved