Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 53 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi 686 2025-06-25

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE K.n.y. MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: -

Je, lini mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kwa ajili ya Kata za Gwanseli, Magata, Muleba, Bureza, Kikuku na Kagoma – Muleba utaanza?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda kwenye Kata Sita za Muleba, Magata/Kurutanga, Gwanseli, Bureza, Kikuku na Kagoma Wilayani Muleba Mkoani Kagera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali inaendelea na utafutaji wa fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo unaokadiriwa kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 42. Aidha, katika mpango wa muda mfupi wa kuboresha huduma ya majisafi na salama katika kata hizo, Serikali imekamilisha utekelezaji wa miradi ya maji minne ya Ilemela, Magata/Kurutanga, Butembo na Kagoma inayohudumia wananchi 22,279 waishio kwenye Vijiji nane vya Ilemela, Gwanseli, Bureza, Butembo, Makarwa, Kikuku, Kagoma na sehemu ya Kijiji cha Nsisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hatua nyingine, Serikali imekamilisha mradi wa upanuzi wa skimu za maji ya Kurutanga na Butembo kwenda Kijiji cha Magata na Kitongoji cha Omdangara, Muleba Mjini ambapo huduma ya maji inawafikia wananchi wapatao 11,340, ahsante.