Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 53 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi 685 2025-06-25

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa Barabara ya Usalimwani - Ikuwo hadi Nkenja kwa kiwango cha changarawe utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Usalimwani – Ikuwo – Nkenja yenye urefu wa klometa 42.7 ni barabara ya Wilaya iliyokasimiwa kwa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mwaka 2023. Ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha changarawe unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 jumla ya shilingi milioni 865.14 zimetumika kufanya matengenezo ya barabara hii ikiwa ni pamoja na kuongeza upana wa barabara, kuweka changarawe, kujenga makalavati pamoja na kuweka zege katika maeneo korofi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika mwaka wa fedha wa 2025/2026 jumla ya shilingi milioni 488.8 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na matengenezo ya barabara hiyo, ikiwa ni pamoja na kuweka changarawe.