Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 53 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 684 2025-06-25

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Handeni – Kiberashi – Kiteto – Mrijo – Chemba – Kwamtoro hadi Singida kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza ujenzi wa Barabara ya Handeni – Kibirashi – Kiteto – Mrijo – Chemba hadi Singida yenye urefu wa kilometa 461 kwa awamu ambapo kwa sehemu ya kwanza Handeni – Mafuleta (kilometa 20) ujenzi umefikia asilimia 46.06.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, sehemu ya pili ya Mafuleta – Kileguru (Km 30) na Kibaya – Kisima (kilometa 50) makandarasi wapo kwenye maandalizi ya kuanza ujenzi. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) wako kwenye majadiliano ya awali ya kuijenga kwa utaratibu wa PPP, ahsante.