Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 53 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi 683 2025-06-25

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilongero

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Igauri Km 11.5 – Ilongero hadi Haydom Km 80 kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Igauri – Ilongero hadi Haydom ni barabara ya mkoa inayojulikana kwa jina la Singida Urban – Ilongero – Haydom (kilometa 93.8). Ujenzi wa Barabara hii kwa kiwango cha lami unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa jumla ya kilometa 12.5 kutoka Singida eneo la Njuki hadi Igauri zimejengwa kwa kiwango cha lami. Aidha, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ipo katika hatua za mwisho za manunuzi ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi kwa sehemu ya Igauri – Ilongero (kilometa 18.5). Kwa sehemu iliyobaki ya kutoka Ilongero hadi Haydom (kilometa 69.8), Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi, ahsante.