Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 53 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 680 2025-06-25

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO K.n.y. MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua Viwanda vya Tanzania Pharmaceutical Industries (TPI) na General Tyre?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango wa kufufua viwanda vyote nchini ambavyo havifanyi kazi kwa sasa ili kujiepusha na gharama kubwa za uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi, upotevu wa ajira, na upotevu wa fedha za kigeni za kuongeza mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kiwanda cha Tanzania Pharmaceutical Industries, kupitia Serikali, Msajili wa Hazina anashirikiana na mwekezaji kukifufua kiwanda hicho, na kwa sasa kipo hatua za mwisho za kuanza ukarabati wa kiwanda pamoja na mitambo; na baada ya ukarabati huo kukamilika, uzalishaji utaanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kiwanda cha General Tyre, Serikali kupitia Shirika la Mandeleo la NDC inatafuta mwekezaji wa kimkakati ili kuanza uzalishaji wa matairi ya magari hapa nchini.