Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 53 Finance Wizara ya Fedha 679 2025-06-25

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI auliza: -

Je, nini faida na hasara ya Tanzania kutokana na msimamo wa Nchi za BRICS ambazo zimejipanga kujiondoa kwenye Mfumo wa Dollarisation?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa na ushirikiano wa karibu wa muda mrefu na nchi za BRICS (Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini) katika nyanja mbalimbali ikijumuisha masuala ya kiuchumi, biashara, na diplomasia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mahusiano hayo yanadumishwa kwa kuendelea kuwepo kwa Balozi za nchi hizo hapa nchini na Tanzania kuwa na Balozi katika nchi hizo. Mahusiano hayo yanaendelea kuleta mafanikio chanya kwa Serikali ya Tanzania kwa kutumia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika nchi hizo ambazo pia zinaimarisha mahusiano ya uwili baina yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Tanzania siyo mwanachama wa BRICS ila inashiriki katika mikutano ya BRICS kama observer. Hivyo, mafanikio au changamoto zozote katika umoja huo zinazoweza kutokea katika sekta ya kiuchumi na fedha hususan ya kujiondoa kwenye Dollarisation, Tanzania hatutakuwa na athari za moja kwa moja kwa kuwa sio wanachama wa BRICS. Ahsante sana.