Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 53 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 678 | 2025-06-25 |
Name
Tunza Issa Malapo
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -
Je, Serikali imejipangaje kudhibiti vumbi la makaa ya mawe yanayosafirishwa kupitia Bandari ya Mtwara?
Name
Khamis Hamza Khamis
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Uzini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Ofisi ya Makamu wa Rais imechukua hatua mbalimbali kwa ajili ya kudhibiti vumbi la makaa ya mawe yanayosafirishwa kupitia Bandari ya Mtwara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua hizo ni pamoja na kuendelea na ujenzi wa bandari nyingine nje ya Manispaa ya Mtwara Mikindani katika eneo la Kisiwa Mgao ambapo bandari hiyo itatumika kusafirisha bidhaa chafuzi kwa mazingira, kama vile simenti na makaa ya mawe. Hivyo, magari yote yanayobeba makaa ya mawe yatapita nje ya Manispaa kuelekea bandarini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua nyingine ni pamoja na kutumia mitambo miwili yenye uwezo wa kupakia tani 600 kwa saa ambayo ina mikanda maalum (Conveyor Belt) kwa ajili ya kupakia mzigo kwenye meli, kuweka nyavu za kuzuia vumbi, kuhakikisha magari yote yanayosafirisha makaa ya mawe yanafunikwa ili kuzuia vumbi lisisambae kwenye mazingira, na kunyunyuzia maji mara kawa mara katika eneo la hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved