Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 53 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 677 | 2025-06-25 |
Name
Vita Rashid Kawawa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Primary Question
MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI K.n.y. MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:-
Je, lini Serikali itatenga bajeti ya ujenzi wa barabara za lami katika mitaa ya Namtumbo?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inafahamu hitaji la barabara za lami katika Mji wa Namtumbo ambazo ni takribani kilomita 28.1, na imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizo kwa awamu, ambapo katika mwaka 2023/2024 kiasi cha shilingi milioni 890 kilitumika kujenga kilomita 1.6 za tabaka la lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2024/2025, Serikali ilijenga barabara yenye urefu wa kilomita 0.5 kwa tabaka la lami kwa gharama ya shilingi milioni 295. Katika mwaka 2025/2026, Serikali imeweka katika mipango yake na bajeti ujenzi wa barabara kwa tabaka la lami yenye urefu wa kilomita moja kwa shilingi milioni 475.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kujenga barabara kwa tabaka la lami katika Mji wa Namtumbo na Makao Makuu ya Miji ya Wilaya zote hapa nchini kulingana na upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved