Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 49 Water and Irrigation Wizara ya Maji 635 2025-06-19

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza kutekeleza Mradi wa Maji Kata ya Uwemba – Njombe Mjini.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza ununuzi wa kumpata Mkandarasi atakayetekeleza Mradi wa Maji Kijiji cha Uwemba uliopo Njombe Mjini. Kazi zinazotarajiwa kutekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 300,000, ulazaji wa mtandao wa bomba umbali wa kilometa 49.8, na ujenzi wa vituo 12 vya kuchotea maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa mradi huo unatarajia kuanza mwanzoni mwa mwaka wa fedha 2025/2026 na utakuwa kwa muda wa miezi nane. Nakushukuru.