Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 49 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 633 2025-06-19

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:-

Je, lini skimu ya umwagiliaji itajengwa katika Kata ya Arusha Chini Moshi Vijijini?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2024/2025 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa skimu mbalimbali nchini, ikiwemo Skimu ya Umwagiliaji ya Chemiko yenye ukubwa wa hekta 2,000 iliyopo katika Kata ya Arusha Chini Moshi Vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Wizara kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika mwaka 2025/2026 itakamilisha usanifu wa skimu hiyo na kuanza taratibu za manunuzi ili kumpata mkandarasi kwa ajili ya ujenzi. Kukamilika kwa ujenzi wa skimu hiyo, kutaongeza tija na uzalishaji wa mazao ya chakula nchini na hivyo kuwanufaisha wakulima wa Kata ya Arusha Chini.