Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 49 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 632 2025-06-19

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:-

Je, lini Jeshi la Zimamoto na Uokoaji litakuwa na Ofisi ya kuendesha shughuli zake katika Wilaya ya Nyasa?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kusogeza huduma za zimamoto na uokoaji karibu na wananchi kwa kujenga vituo vya zimamoto na uokoaji. Katika mwaka 2025/2026, Serikali kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji imetenga kiasi cha fedha shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo cha Zimamoto na Uokoaji katika Wilaya mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mpango wa ujenzi wa vituo vya zimamoto na uokoaji katika Wilaya zote nchini ikiwemo Wilaya ya Nyasa.