Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 49 | Works, Transport and Communication | Wizara ya Ujenzi | 630 | 2025-06-19 |
Name
Oran Manase Njeza
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbeya Vijijini
Primary Question
MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, je, Serikali inaonaje umuhimu wa kuchukua mikopo kwenye taasisi mbalimbali ili waweze kuwafungia wananchi ambao hawana uwezo wa kulipa kwa mkupuo mmoja shilingi 320,000.00 mpaka 350,000.00, halafu baadaye wakaweka kwenye gharama za kutoa umeme kwa hawa wateja wakawa wanalipa kidogo kidogo? Je, Serikali inasemaje kuhusu hoja hiyo. (Makofi)
Name
Abdallah Hamis Ulega
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkuranga
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha kwamba Serikali inaunganisha umeme kwa wananchi wengi, jitihada mbalimbali zimechukuliwa na Serikali kuhakikisha kwamba jambo hili linafanyika vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama Waheshimiwa Wabunge wanavyofahamu, tumepiga hatua kubwa ya kuhakikisha kwamba vijiji vyote nchini vimeweza kuunganishwa na umeme, na sasa tunakwenda kwenye eneo la vitongoji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maarifa yoyote yatakayotuwezesha kuhakikisha kwamba tunawaunganisha wananchi wetu kwa ukubwa na kwa ukamilifu, Serikali itayaangalia kuona uwezekano wake wa kutekeleza na pale inapoonekana inawezekana, tutafanya hivyo. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved