Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 41 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 532 | 2025-06-06 |
Name
Constantine John Kanyasu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Geita Mjini
Primary Question
MHE. TUMAINI B. MAGESSA K.n.y. MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -
Je, upi mpango wa Serikali kuokoa maisha ya wananchi kutokana na uwepo wa ajali nyingi katikati ya Mji wa Geita maeneo ya Nyankumbu na Shilabela?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Mkoa wa Geita kwa kushirikiana na TANROADS pamoja na Jeshi la Polisi wamekubaliana kuendelea kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya barabara kwa wananchi na madereva wa vyombo vya moto. Katika eneo la Nyankumbu yamewekwa matuta pamoja na alama ya mwendokasi wa kilometa 50 kwa saa ili kupunguza ajali na kuokoa maisha ya wananchi kwa kuwa eneo hili pamoja na eneo la Shilabela ni maeneo yenye watu wengi na shughuli nyingi za kiuchumi. Aidha, Serikali kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji inaendelea na utoaji wa elimu kwa umma juu ya kinga na tahadhari dhidi ya majanga mbalimbali katika mji wa Geita. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved