Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 41 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 531 | 2025-06-06 |
Name
Tamima Haji Abass
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza: -
Je, Serikali ina mkakati gani wa kutoa elimu kwa wajasiriamali wadogo ili kuwawezesha kuwa na vifungashio bora vya bidhaa zao? (Makofi)
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Viwanda (SIDO) inatekeleza mkakati wa mafunzo ya ufungashaji wa bidhaa kwa wajasiriamali ikiwemo namna ya kutengeneza vifungashio, kutumia chapa (brand) na label. Vilevile SIDO inatoa elimu kwa waundaji (designers) na wachapaji wa label za bidhaa ili kuwaongezea ujuzi katika kuwahudumia wajasiriamali. Lengo la mafunzo hayo ni kuboresha vifungashio vya bidhaa za wajasiriamali ili ziweze kushindana sokoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, SIDO hununua vifungashio kwa jumla (bulk procurement) kutoka nje ya nchi na kuviuza kwa rejareja na kwa bei nafuu katika Ofisi za SIDO za Mikoa kwa wajasiriamali. Hatua hiyo huwawezesha wajasiriamali kupata vifungashio bora na kwa bei nafuu, nakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved