Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 41 Finance Wizara ya Fedha 530 2025-06-06

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -

Je, Serikali imepiga hatua gani katika kurasimisha biashara za sekta isiyo rasmi ili kuongeza uchumi wa nchi?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, Serikali kupitia TRA ina utaratibu wa kuwatambua walipakodi kulingana na mitaa (Blocks Management System) ambayo husimamiwa na maofisa kodi ambao hutembelea mitaa husika na kufanya ukaguzi kwa wafanyabiashara ili kujua mwenendo wao katika kulipa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Serikali kupitia TRA imeendelea kuwatambua na kuwasajili wafanyabiashara wadogo wadogo pamoja na kuwapa elimu juu ya huduma za kikodi ikiwa ni pamoja na TIN.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha, TRA, TAMISEMI, Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maendeleo na Makazi na Mifuko ya Kijamii na Wizara ya Viwanda, ipo katika zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya kijiditali kwa wafanyabiashara ndogo ndogo kwa lengo la kuwatambua, kuwawezesha kimitaji na kufuatilia kwa karibu maendeleo ya biashara zao. Lengo la mkakati huu ni kuwakuza wafanyabiashara na hatimaye kuwaingiza kwenye mfumo rasmi ambao wataweza kusajiliwa na kulipa kodi, ahsante sana. (Makofi)