Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 49 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 628 2025-06-19

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatatua tatizo la kukosa huduma ya umeme katika Vitongoji vya Jimbo la Tabora Mjini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Tabora Mjini lina jumla ya Vitongoji 159 ambapo kati ya hivyo, vitongoji 69 vimepatiwa umeme, vitongoji 15 Wakandarasi wanaendelea na utekelezaji wa miradi kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Kwanza, na vitongoji 24 zabuni imetangazwa ili kupata Wakandarasi wa kutekeleza miradi kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili. Vitongoji 51 vilivyosalia vitapelekewa umeme kulingana na upatikanaji wa fedha.