Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 49 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 628 | 2025-06-19 |
Name
Emmanuel Adamson Mwakasaka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tabora Mjini
Primary Question
MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -
Je, lini Serikali itatatua tatizo la kukosa huduma ya umeme katika Vitongoji vya Jimbo la Tabora Mjini?
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Tabora Mjini lina jumla ya Vitongoji 159 ambapo kati ya hivyo, vitongoji 69 vimepatiwa umeme, vitongoji 15 Wakandarasi wanaendelea na utekelezaji wa miradi kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Kwanza, na vitongoji 24 zabuni imetangazwa ili kupata Wakandarasi wa kutekeleza miradi kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili. Vitongoji 51 vilivyosalia vitapelekewa umeme kulingana na upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved