Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 41 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo 527 2025-06-06

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwanja cha michezo (centre of excellence) Manispaa ya Ilemela chenye hekari 16.75 ambacho kina hati tayari?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina dhamira ya dhati ya kuendeleza eneo hilo. Hata hivyo kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele katika kukamilisha miradi ya ujenzi wa miundombinu ya michezo ambayo itatumika kuendeshea mashindano ya CHAN 2025 na AFCON 2027. Aidha, Serikali imeanza ujenzi wa akademia ya michezo katika Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya kilichopo Wilaya ya Kwimba, mkoani Mwanza ambapo utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 25.4. Hivyo kwa kuanzia, wananchi wa Mkoa wa Mwanza watanufaika na mradi huo mara utakapokamilika, huku tukiendelea kujipanga na utekelezaji wa mradi katika Manispaa ya Ilemela.