Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 41 | Lands, Housing and Human Settlement Development | Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi | 526 | 2025-06-06 |
Name
Dr. Christine Gabriel Ishengoma
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -
Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza migogoro ya wafugaji na wakulima Mkoani Morogoro?
Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kuwepo kwa migogoro ya wafugaji na wakulima Mkoani Morogoro. Hata hivyo, Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kukabiliana na migogoro hiyo ambapo baadhi ya hatua hizo ni pamoja na kuweka mipango ya matumizi bora ya ardhi za vijiji ili kubainisha maeneo ya kilimo sambamba na maeneo ya wafugaji kupitia Tume ya Taifa ya Matumizi Bora ya Ardhi. Aidha, hatua nyingine ni kupitia Mradi wa KKK ambapo miji chipukizi kama ilivyo kwa miji ya halmashauri kupangwa, kupimwa na kumilikishwa sambamba na kuweka mipango ya matumizi bora ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa wananchi kuhakikisha kuwa wanatumia ardhi kuendana na mipango ya matumizi iliyopangwa ili kuondoa muingiliano wa matumizi ya ardhi ambayo imekuwa ni chanzo cha migogoro ya wakulima na wafugaji.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved