Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 41 Water and Irrigation Wizara ya Maji 525 2025-06-06

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali juu ya changamoto ya maji maeneo ya Jimbo la Kinondoni hususani Kata za Mwananyamala na Makumbusho?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha maeneo yote ya Jiji la Dar es Salaam yanapata huduma ya majisafi, salama na yenye kutosheleza, zikiwemo Kata za Mwananyamala na Makumbusho. Kata hizo zimekuwa na ongezeko kubwa la watu huku miundombinu yake ya maji ikiwa ni ya muda mrefu na inakabiliwa na changamoto ya uchakavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026 itakarabati miundombinu ya maji katika eneo la Kisiwani Msikitini, kwa ajili ya kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji katika maeneo yote ya Kata za Mwananyamala na Makumbusho, ahsante sana.