Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 41 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 524 | 2025-06-06 |
Name
Jacquline Andrew Kainja
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MARTHA F. MARIKI K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: -
Je, lini tatizo la maji litamalizwa kwa maeneo yasiyo na mito, mabwawa au mradi wa maji ya Ziwa Victoria hasa Kijiji cha Kiomboi, Kitongoji cha Madole Sita?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha vijiji vyote vinafikiwa na huduma ya majisafi, salama na yenye kutosheleza. Katika kutekeleza azma hiyo, Serikali inatekeleza programu ya uchimbaji wa visima vitano kwenye kila jimbo, hususan kwenye vijiji visivyokuwa na huduma ya maji nchini. Kupitia programu hiyo Kitongoji cha Madole Sita kilichopo Kijiji cha Kiomboi, Wilayani Sikonge kitachimbiwa kisima kirefu, kwa ajili ya kutoa huduma ya maji kwa wananchi wa eneo hilo ambapo kwa sasa kazi ya utafiti wa maji chini ya ardhi inaendelea. Aidha, Serikali inaendelea na mradi wa utafiti wa maji ardhini na uchimbaji wa visima 17 katika vijiji vyote ambavyo havijafikiwa na huduma ya maji Wilayani Sikonge.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved