Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 41 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 523 | 2025-06-06 |
Name
Hassan Zidadu Kungu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduru Kaskazini
Primary Question
MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha mradi wa maji katika Kata ya Kalulu ili kumtua mama ndoo kichwani na kutimiza ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026 itaanza utekelezaji wa mradi wa maji wa Kata ya Kalulu uliopo Wilayani Tunduru, Mkoa wa Ruvuma. Kazi zinazotarajiwa kutekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa nyumba mbili za mitambo (pump house), ufungaji wa pampu za kusukuma maji, ujenzi wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 50,000 kila moja, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 13, sanjari na ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji vya malipo ya kabla. Mradi huo unatarajiwa kunufaisha zaidi ya wananchi 4,715 waishio katika vijiji viwili vya Rahaleo na Mbungulaji vilivyopo katika Kata ya Kalulu.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved