Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 41 | Union Affairs | Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano | 522 | 2025-06-06 |
Name
Zahor Mohamed Haji
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwera
Primary Question
MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: -
Je, ni lini Serikali italeta muswada wa sheria kuhusu changamoto za Muungano zilizopatiwa ufumbuzi ili sasa ziwe kwa mujibu wa sheria?
Name
Khamis Hamza Khamis
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Uzini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa mpaka sasa jumla ya changamoto 22 za Muungano zimekwishapatiwa ufumbuzi. Aidha, katika Kikao cha Kamati ya Pamoja ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SJMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ambacho kilifanyika tarehe 4 Aprili, 2025 Ikulu Dar es Salaam kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa changamoto za Muungano, kilitoa maelekezo kwa Ofisi za Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kulifanyia kazi jambo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, mara baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa taarifa hiyo, itatolewa kwa umma, ninakushukru.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved