Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 49 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 626 | 2025-06-19 |
Name
Jesca Jonathani Msambatavangu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Iringa Mjini
Primary Question
MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: -
Je, kwa nini Pensheni hazibadiliki na kupanda kutokana na mfumuko wa bei?
Name
Ridhiwani Jakaya Kikwete
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chalinze
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kupanda kwa pensheni hutegemea hali ya uhimilivu wa mifuko. Serikali hufanya tathmini ambayo matokeo ya tathmini hizo huwezesha kujua mifuko kama ni himilivu na ina uwezo wa kuhuisha pensheni za wastaafu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuboresha mafao, Serikali kupitia Mifuko ya Hifadhi ya Jamii imepandisha kiwango cha Pensheni kutoka shilingi 100,000.00 hadi kufikia shilingi 150,000.00 kwa mwezi, kuanzia mwezi Januari, 2025, na pia kuhuisha pensheni kwa wastani wa asilimia mbili kwa kuzingatia mfumuko wa bei. Serikali itaendelea kuhuisha pensheni kadri uhimilivu wa mifuko yetu unavyoendelea kuimarika.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved