Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 37 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 483 | 2025-06-02 |
Name
Fatma Hassan Toufiq
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga reli ya kisasa kutoka Kituo Kikuu cha SGR Dodoma hadi Uwanja wa Ndege Msalato?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) imekamilisha upembuzi yakinifu kwa ajili ya Ujenzi wa Reli ya Kisasa katika Jiji la Dodoma (Dodoma Commuter Train). Ujenzi wa Reli hiyo unalenga kuimarisha usafiri katika Jiji la Dodoma kwa kuunganisha Jiji na viunga vyake ikiwemo Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa Serikali ipo katika hatua za utafutaji wa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa reli hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved