Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 37 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 483 2025-06-02

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga reli ya kisasa kutoka Kituo Kikuu cha SGR Dodoma hadi Uwanja wa Ndege Msalato?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) imekamilisha upembuzi yakinifu kwa ajili ya Ujenzi wa Reli ya Kisasa katika Jiji la Dodoma (Dodoma Commuter Train). Ujenzi wa Reli hiyo unalenga kuimarisha usafiri katika Jiji la Dodoma kwa kuunganisha Jiji na viunga vyake ikiwemo Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa Serikali ipo katika hatua za utafutaji wa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa reli hiyo.