Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 37 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 477 | 2025-06-02 |
Name
Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba kusini
Primary Question
MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: -
Je, kwa nini watumiaji wa Daraja la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wanalipia kila wanapopita huku watumiaji wa Daraja la Tanzanite hawalipi? (Makofi)
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, watumiaji wa Daraja la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wanalipia kila wanapopita kwa sababu daraja hili limejengwa kwa utaratibu wa ubia (Public Private Partnership - PPP) ambapo mwekezaji hurudisha fedha zake alizowekeza pamoja na faida kutokana na tozo kwa watumiaji. Kwa upande wa Daraja la Tanzanite watumiaji hawalipi kwa sababu daraja hilo limejengwa kwa utaratibu wa kawaida kama uliotumika kujenga madaraja mengine nchini.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved