Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 37 Planning and Investment Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji). 475 2025-06-02

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha Ilani za Uchaguzi za Vyama vya Siasa zinaendana na Dira ya Taifa?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchakato wa maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo umeshirikisha wadau mbalimbali ikiwemo vyama vya siasa. Kwa mfano, mnamo tarehe 21 Agosti, 2024 Msajili wa Vyama vya Siasa aliandaa kikao cha vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu nchini, kwa lengo la kuwapa nafasi viongozi wa vyama hivyo kutoa maoni yao kuhusu Rasimu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kikao hiki pamoja na mambo mengine, viongozi wa vyama vya siasa walitoa maoni na kukubaliana kuwa maudhui ya Ilani ya vyama vyao kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 yaakisi maudhui ya Dira 2050. Hivyo, Serikali inaamini kuwa vyama vya siasa vitazingatia makubaliano yao na kutumia kikamilifu maudhui ya Rasimu ya Dira 2050 katika kuandaa Ilani ya vyama vyao vya siasa, ahsante.