Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 37 | Finance | Wizara ya Fedha | 480 | 2025-06-02 |
Name
Prof. Patrick Alois Ndakidemi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Moshi Vijijini
Primary Question
MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: -
Je, Serikali imejiandaa vipi kukabiliana na mabadiliko ya sera za baadhi ya nchi tajiri kulisaidia Taifa letu kukuza uchumi?
Name
Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Iramba Magharibi
Answer
WAZIRI WA FEDHA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na jitihada mbalimbali za kuongeza mapato ya ndani ili kuhakikisha kuwa sehemu kubwa ya bajeti inagharamiwa kwa kutumia mapato ya ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, kwa kutambua umuhimu wa mahitaji ya kibajeti ikiwemo ugharamiaji wa miradi ya maendeleo, Serikali itaendelea kuvutia ushiriki wa sekta binafsi katika ugharamiaji wa miradi ya maendeleo kwa kutumia njia mbadala ikiwemo ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi. Hii itasaidia kuipunguzia Serikali mzigo wa kukopa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kupunguza utegemezi wa kibajeti kutoka kwa Washirika wa Maendeleo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved