Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 45 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 584 2025-06-12

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti ongezeko la Wagonjwa wa Kansa nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali katika kukabiliana na ongezeko la wagonjwa wa Kansa kwa kufanya yafuatayo: -

(a) Kutoa elimu kwa umma kuhusu kujikinga na ugonjwa wa saratani kupitia vipindi vya redio, televisheni, machapisho, magazeti na mitandao ya kijamii;

(b) Serikali inatoa chanjo ya Human Papilloma Virus kwa wasichana ili kuwakinga na kirusi kinachosababisha saratani ya mlango wa kizazi;

(c) Kuanzisha huduma za awali za uchunguzi na matibabu ya saratani kuanzia ngazi ya zahanati hadi hospitali za Taifa;

(d) Serikali imeimarisha huduma za kibingwa za uchunguzi na matibabu kwa kuhakikisha uwepo wa wataalamu na vifaa tiba kwa ajili ya kukabiliana na Saratani.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.