Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 45 Water and Irrigation Wizara ya Maji 581 2025-06-12

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mradi wa Maji Kata ya Songambele, Kyerwa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha huduma ya majisafi na salama inapatikana kwa wananchi wote waishio vijijini, wakiwemo wananchi wa Kata ya Songambele iliyopo Wilayani Kyerwa, Mkoa wa Kagera. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali kupitia mpango wa muda mfupi wa Programu Maalum ya Uchimbaji wa Visima 900, imekamilisha uchimbaji wa kisima kirefu pamoja na ujenzi wa miundombinu rahisi ya kutolea huduma kwa wananchi (point source) katika Kijiji na Kata ya Songambele na wananchi wanapata huduma. Aidha, katika mpango wa muda mrefu, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026 itaanza kutekeleza awamu ya kwanza ya mradi wa usambazaji maji katika Vijiji vya Kata ya Songambele.

Mheshimiwa Spika, miongoni mwa kazi zinazotarajiwa kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 300,000, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 21 sanjari na ujenzi wa vituo 23 vya kuchotea maji. Mradi huo unatarajiwa kutekelezwa ndani ya miezi nane, ambapo utanufaisha zaidi ya wananchi 18,404 waishio kwenye Vijiji vya Kata ya Songambele. (Makofi)