Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 37 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 473 | 2025-06-02 |
Name
Rehema Juma Migilla
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Ulyankulu
Primary Question
MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: -
Je, lini Serikali itatenga fedha za ujenzi wa Daraja linalounganisha Kijiji cha Mwanduti na Ibambo katika Kata ya Mwongozo?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha usanifu wa awali wa daraja linalounganisha Kijiji cha Mwanduti na Ibambo. Aidha, usanifu wa kina umepangwa kufanyika katika mwaka wa fedha 2025/2026 kwa lengo la kubaini gharama halisi za ujenzi, mahitaji ya kiufundi na maandalizi ya nyaraka za zabuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya usanifu wa kina kukamilika, Serikali itatafuta fedha za ujenzi wa daraja hilo ili kutatua changamoto ya mawasiliano katika Vijiji vya Mwanduti na Ibambo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved