Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 37 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 471 | 2025-06-02 |
Name
Zuena Athumani Bushiri
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Wodi za Wanaume na Wanawake katika Hospitali ya Wilaya ya Same?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilianza ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Same, Novemba, 2022. Hadi mwezi Aprili, 2025 Serikali imepeleka jumla ya shilingi bilioni 3.4, ambapo shilingi bilioni 2.6 zimetumika katika ujenzi wa majengo ya hospitali ya halmashauri hiyo na shilingi milioni 800 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba. Aidha, majengo matano kati ya nane, ujenzi umekamilika na yameanza kutoa huduma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026 imetenga shilingi milioni 800, kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wanaume, wanawake, watoto na ujenzi wa njia za kutembea wagonjwa (Walkways) katika Hospitali ya Wilaya ya Same, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved