Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 37 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 470 | 2025-06-02 |
Name
Iddi Kassim Iddi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Msalala
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: -
Je, lini Serikali itaielekeza Halmashauri ya Msalala kuanza kulipa posho za Wenyeviti wa Vijiji?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ina jumla ya vijiji 92 ambavyo vyote vina Wenyeviti wa Vijiji. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Halmashauri ya Msalala ilitenga shilingi milioni 5.5, kwa ajili ya posho za Wenyeviti wa Vijiji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025, halmashauri ilitenga shilingi milioni 11.04. Hadi Mei, 2025, shilingi milioni 10.1 zimelipwa na kiasi cha shilingi 920,000 kitalipwa kufikia Juni, 2025.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali imetenga shilingi milioni 11.04, kwa ajili ya kuendelea kulipa posho za Wenyeviti wa Vijiji katika Halmashauri ya Msalala, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved